Matonya kizimbani kwa madai ya unyanyasaji wa kingono

Share this story

Msanii wa Tanzania, Sefu Shabani 43, anayejulikana zaidi kama Matonya amekamatwa na kushtakiwa nchini Kenya kwa madai ya unyanyasaji wa kingono

Matonya, ambaye amewahi kutamba na nyimbo maarufu kama ‘Vaileti’ na ‘Anita’, amekanusha tuhuma zote zinazomkabili Mahakamani hapo.

Baada ya kusomewa mashtaka, Mahakama imemruhusu kuwa nje kwa dhamana, huku ikiweka masharti ya kukabidhi hati yake ya kusafiria Mahakamani.

Aidha, Msanii huyo amezuiliwa kusafiri nje ya eneo husika bila kupata kibali rasmi kutoka Mahakama hiyo hadi kesi yake itakaposikilizwa na kuamuliwa.


Share this story

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Previous post Taita Taveta Kicks Off Key KDSP II Performance Assessment
Next post “Finale Yavunja Rekodi: Bien Aelezea Mafanikio Makubwa Zaidi”