Hofu Kivuko Cha Likoni Baada Ya Mwanaume Mmoja Kukamatwa Akiwa Na Kitu Kilichoonekana Kama Bunduki
Hofu iliongezeka katika Kivuko cha Likoni, Mombasa, baada ya mwanamume mmojai kukamatwa akiwa amebeba kitu kilichoonekana kama bunduki, hali iliyowafanya maafisa wa usalama kuchukua hatua za haraka.
Katika video iliyosambaa mitandaoni, maafisa walionekana wakimzunguka mwanamume huyo, aliyekuwa amevaa magunia na nguo chakavu, na kumfanyia upekuzi wa kina, jambo lililozua wasiwasi miongoni mwa wananchi kuhusu usalama.
Hata hivyo, akizungumzia tukio hilo, Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi, Gilbert Masengeli, alifafanua kuwa mwanamume huyo hakuwa na bunduki halisi bali ya kuchezea. Kulingana na Masengeli, mtu huyo alibainika kuwa na matatizo ya akili na alipelekwa hospitalini kwa uchunguzi wa kitabibu.