Anerlisa Muigai Arejea Mitandaoni Baada ya Mda Mrefu
Mfanyabiashara wa Kenya, Anerlisa Muigai, amerejea rasmi kwenye mitandao ya kijamii baada ya kipindi kirefu cha ukimya, akichagua tukio maalum kuashiria kurejea kwake.
Anerlisa alionekana tena mtandaoni wakati wa kusherehekea siku ya kwanza ya kuzaliwa kwa mwanawe, Kasen Muigai, tukio lililogusa hisia za wengi na kuvutia hisia chanya kutoka kwa wafuasi wake.

Kwa miezi kadhaa iliyopita, mfanyabiashara huyo alikuwa amepunguza kwa kiasi kikubwa uwepo wake mtandaoni, hali iliyowaacha mashabiki wake na maswali mengi kuhusu maisha yake ya sasa.
Anerlisa aliwahi kupata umaarufu mkubwa nchini Tanzania wakati wa uhusiano wake na mwanamuziki wa Bongo Flava, Ben Pol, ambapo inadaiwa walifikia hatua ya kufunga ndoa.
Kurejea kwake sasa kumeibua upya mjadala miongoni mwa mashabiki, wengi wakionyesha furaha yao kumuona akirejea na kushiriki tena maisha yake hadharani.