Shilingi Ya Kenya Yaendelea Kufanya Vizuri Zaidi Ya Sarafu Zingine Ulimwenguni

Share this story

Shilingi ya Kenya imekuwa fedha inayofanya vizuri zaidi duniani katika muda wa chini ya miezi mitatu. Hii ni baada ya kupata kwa asilimia 20, ikimshinda Rupia ya Sri Lanka ambayo imeimarika kwa asilimia 6.1.

Tangu Februari Shilingi imeendelea kupata faida kubwa dhidi ya dola. Kufikia Alhamisi, Machi 14, Shilingi ya Kenya ilikuwa ikibadilishwa kuwa 137.49 kwa kila dola ya Marekani kulingana na Benki Kuu ya Kenya.

Sababu zinayochangia ni utozaji wa ziada wa Bondi za Hazina ikiwa ni pamoja na bondi za miundombinu zenye thamani ya Ksh70 bilioni zilizotolewa na Benki Kuu ya Kenya Januari mwaka huu.

Hazina ya Kitaifa ilichangisha Ksh241 bilioni kutoka kwa wawekezaji wa kigeni walionunua dhamana za miundombinu. Usajili wa ziada katika hati fungani za serikali ulihusishwa na imani ya wawekezaji katika mikakati ya kiuchumi na usimamizi wa madeni ya Kenya. Vile vile, ongezeko la utumaji wa pesa kutoka kwa Wakenya wanaoishi ughaibuni lilichangia faida ya shilingi.


Share this story

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Previous post Cha Mackenzie Bado Jikoni, Mahakama Yakataa Kumwachilia Kwa Dhamana
Next post Jamaica Dancehall Star Vybz Kartel Wins Appeal Over Murder Conviction.