ISAK ATANGAZA KUHITIMISHA SAFARI YAKE NEWCASTLE

Share this story

Alexander Isak amethibitisha kuwa hatavaa tena jezi ya Newcastle United.

Hata kama dirisha la usajili litafungwa bila yeye kuondoka, nyota huyo wa Sweden anaona muda wake na klabu hiyo umefika mwisho na hatarajii kurejea tena kwenye kikosi.

Hata hivyo, Newcastle wamesisitiza kuwa hawana mpango wa kumuuza, ingawa wapo kwenye mchakato wa kutafuta mbadala wake sokoni.

Inadaiwa Isak alishaweka wazi tangu msimu uliopita kuwa ulikuwa wa mwisho kwake St James’ Park, na tayari amemwambia kocha Eddie Howe kuhusu nia yake ya kuondoka. Liverpool ilishatuma ofa ya pauni milioni 110 ikakataliwa, lakini Newcastle huenda ikakubali iwapo dau litakaribia pauni milioni 150.

Chanzo: David_Ornstein


Share this story

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Previous post CAF strongly condemns security breaches at Kasarani Stadium during Kenya National Team matches
Next post CAF Disciplinary Board hits Kenya with fines over CHAN 2024 Security breaches.