Kaunti ya Mombasa Yarekebisha Mpango wa Bursary Baada ya Kukubaliana na Serikali ya Kitaifa
Serikali ya Kaunti ya Mombasa imetangaza mageuzi katika mpango wake wa ufadhili wa masomo kufuatia makubaliano mapya na Serikali ya Kitaifa na mamlaka ya shule za umma. Katika taarifa ya Jumamosi, Februari 7, Gavana Abdulswamad Sheriff Nassir alisema kaunti imerekebisha mfumo wake wa malipo ili kujumuisha kipengele cha lishe shuleni kwa shule zote za sekondari za kutwa za umma. “Serikali ya Kaunti ya Mombasa imepiga hatua kubwa katika kuwezesha elimu ya upili kuwa nafuu zaidi kwa kurekebisha mpango wake wa masomo ili kujumuisha sehemu ya kulisha shuleni kwa shule zote za upili za kutwa za umma.
Abdulswamad alibaini kuwa mpango huo utaanza mara moja