
Hospitali kuu ya Pwani yatangaza kufungwa kwa lango kuu kwa miezi 3
Hospitali kuu ya Rufaa ya Pwani imetangaza kufunga kwa muda lango lake kuu.
Hatua hiyo itasaidia kuwezesha ukarabati ulioratibiwa wa CGTRH.
Eneo lingine litakalo fungwa kwa muda ni pamoja na eneo la usajili, kituo cha uzazi, eneo la majeruhi/ OPD na kitengo cha Meno.
Wagonjwa wameshauriwa kutumia lango la majeruhi kupata hospitali.