KQ yasitisha safari za ndege kwenda UAE kutokana na kufungwa kwa anga
Shirika la ndege la Kenya Airways limesitisha safari za ndege kuelekea Dubai na Sharjah kufuatia kufungwa kwa anga ya Umoja wa Falme za Kiarabu kutokana na vita kati ya Marekani, Israel na Iran. Katika taarifa, KQ ilitangaza kughairi safari za ndege za KQ310, KQ305 na za mizigo, ikitaja hatua hiyo kama hatua ya usalama kwa wateja na wafanyakazi wake.