Serikali ya Tanzania Yawataka Wananchi Kusalia Majumbani Siku ya Uhuru
Serikali ya Tanzania imewashauri raia kubaki majumbani mwao wakati wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru mwaka huu huku hali ya wasiwasi ya usalama ikiongezeka kabla ya maandamano ya kupinga serikali yanayopangwa kufanyika nchini kote tarehe 9 Disemba. Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba alitoa agizo hilo wakati akitoa ujumbe wa sikukuu ya Rais Samia Suluhu Hassan, akisema wafanyakazi muhimu pekee ndio wanaopaswa kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi.
Tangazo hilo limekuja siku moja baada ya Nchemba kuwataka wananchi kuepuka maandamano hayo ambayo wanaharakati wa haki za binadamu na makundi ya upinzani wameyaitisha kujibu tuhuma za ukiukwaji wa haki za binadamu baada ya uchaguzi wa Oktoba wenye utata. “Ndugu zangu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, anawatumia salamu za rambi rambi Watanzania wote tunapoadhimisha Siku ya Uhuru wa Tanzania Bara Desemba 9,” alisema.