
Sudan Yavunja Uhusiano Na UAE
Sudan imetangaza kuwa itavunja uhusiano na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), baada ya jeshi kuituhumu UAE kuunga mkono kikosi pinzani cha Rapid Support Forces (RSF) katika vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea nchini humo.
Baraza la Ulinzi la Sudan limedai UAE imekuwa ikiwapa RSF silaha za kisasa zilizowasaidia kushambulia maeneo muhimu katika jiji la Port tangu Jumapili.