
Nandy Aachana Na Yammy
Nandy amethibitisha ya kuwa Yammy hatokuwa tena msanii wake chini ya Label ya THE AFRICAN PRINCES kwa makubaliano ya Kirafiki baina ya pande mbili . Nandy ameongeza kuwa, Yammy ameondoka ili kuwapa nafasi wasanii wengine.
Maamuzi haya yameibua maswali kwa wadau ambao wamemjibu Nandy kuwa ” HAKIKA WANAWAKE HATUPENDANI” wengine wakahusisha kuwa huenda Nandy kaogopa mme wake asijekukosea njia na kwenda kwa Yammy ambaye anasifika kwa Kitovu kizuri.
Yammy kafuta picha na video zote alizopiga akiwa kwenye Label hali iliyozua maswali kuwa huenda hajaondoka kwa amani
Unadhani ni sahihi Nandy kumuachia Yammy mda huu?
Je Yammy atasikika tena au ndo basi kama Mbosso?